STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, February 4, 2011

Extra Bongo yaivunjavunja Twanga Pepeta





NENO zuri la kusema ni kwamba African Stars 'Twanga Pepeta' imevunjwavunjwa baada ya wanamuziki wake nyota saba kuihama bendi hiyo kwa mpigo na kutua Extra Bongo 'Wana 'Next Level' iliyoingia rasmi kambini kujiwinda na albamu mpya ya pili.
Wanamuziki hao saba walitambulishwa rasmi leo asubuhi na Mkurugenzi wa Extra Bongo, Ally Choki, ambapo alisema lengo la kuwanyakua wakali hao ni kutaka bendi yake iwe matawi ya juu na kuleta mabadiliko ya muziki wa dansi nchini.
Choki aliwatambulisha wanamuziki hao ambapo ni waimbaji wawili, wapiga gitaa wawili na madansa watatu akiwemo mkali Hassani Mussa 'Super Nyamwela'.
Mbali na Nyamwela aliyeitumikia Twanga kwa miaka 11 mfululizo bila kuhama ni Rogart Hegga 'Catapilla' na Saul Ferguson ambao ni waimbaji, Hosea Mgohachi mpuiga gita zito la besi na Godi Kanuti anayecharaza magita yote.
Wanenguaji wengine waliomfuata Nyawela Extra Bongo ni Otilia Boniface na Issack Burhan maarudu kama Danger Boy.
Choki alisema wanamuziki hao wote wana mikataba na bendi yao na mchana huu wanatarajia kuungana na wanamuziki wenzao kambini eneo la Mbezi Mwisho kujipanga kwa albamu mpya.
Alisema kambi hiyo ya muda wa wiki tatu itatumika kuwapa fursa wanamuziki hao wapya kuzoeana na wenzao kabla ya kuanza kufanya vitu vyao hadharani wakiwa wamezaliwa upya.
Mkurugenzi huyo aliyesema tukio kama hilo la kuibomoa Twanga liliwahi kumtokea miaka minne iliyopita alipochukuliwa wanamuziki wa idadi kama hiyo na ASET na kuifanya Extra Bongo 3x3 Kujinafasi kuzimika hadi ilipofufuka mwaka jana.
Alisema wanamuziki hao wapya wamenyakuliwa na Extra Bongo tayari kuziba nafasi za waliotemwa akiwemo rapa machachai Greyson Semsekwa na wenzake kadhaa.
Wakizungumza kwenye utambulisho huo, Ferguson na Nyamwela walisema wamekuja kuthibitisha thamani yao na mashabiki wa Extra Bongo watarajie makubwa.
"watarajie kazi bab'kubwa kwani tunafahamika kwa vipaji vya fani hii," alisema Ferguson.

No comments:

Post a Comment