STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, February 22, 2011

Dokii ana scandal na JB



MSANII nyota wa muziki na filamu, Ummy Wenceslaus 'Dokii' amefyatua kazi yake mpya iitwayo 'Scandal' iliyowashirikisha wakali kadhaa wa fani hiyo nchini.
Filamu hiyo inayozungumzia masuala ya mapenzi na hila za baadhi ya watumishi wa Mungu, inatarajiwa kuachiwa mitaani kuanzia mwezi ujao ikiwa imetungwa na Dokii mwenyewe na kuongozwa na Adam Kuambiana.
Akizungumza na micharazo, Dokii, aliyeng'ara na michezo ya kuigiza kupitia kituo cha ITV akiwa na kundi la Mambo Hayo, alisema ndani ya filamu hiyo aliyoitunga mwenyewe, kuna wasanii mahiri kama Jacob Stephen 'JB'.
"Baada ya kimya tangu nilipoachia filamu ya Money Transfer, nimekamilisha kazi mpya iitwayo Scandal' ambayo nimeigiza na wasanii kadhaa nyota akiwemo mkali, JB, Colleta Raymond, Tini White na wengine," alisema Dokii.
Dokii aliwataja wasanii wengine waliopo ndani ya filamu hiyo ni pamoja na Jacqueline Pentezel 'Jack wa Chuz', Ramadhani Ally 'Taff', Tini White, Kishoka na wengine.
"Ni filamu ya kusisimua kwa jinsi ilivyoigizwa na ujumbe uliopo ndani ya kazi hiyo mpya," alisema Dokii.
Dokii, ambaye pia ni muimbaji wa muziki wa Injili amewahi kutamba na filamu kama Yoland, Hard Love Moro, Bad Friend, My Nephew, Lonely Heart na nyinginezo.
Kwa muda mrefu msanii huyo alikuwa wakiwachanganya mashabiki wake wakidhani ni Mkenya kutokana na kupenda kwake kuigiza lafudhi ya taifa hilo, ingawa ukweli yeye ni mwenyeji wa mkoa wa Morogoro.

Mwisho

No comments:

Post a Comment