STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, February 22, 2011

Aisha Bui: Kisura anayetamba Bongo Movie




HANA muda mrefu tangu atumbukie kwenye faini ya uigizaji, lakini makali yake kupitia baadhi ya kazi alizoshiriki, zimemfanya Aisha Fat'hi maarufu kama Aisha Bui, kuwa tishio kwa waigizaji wakongwe wa kike.
Mwenyewe anakiri aliingia rasmi kwenye fani hiyo mwaka juzi kutokana na kuvutiwa na Wema Sepetu, licha ya kudai alipenda uigizaji licha ya kutowahi kujaribu tangu alipokuwa mdogo.
"Wema ndiye aliyechangia kujiingiiza kwangu kwenye filamu kutokana na kuvutiwa nae, ila tangu utotoni nilikuwa naipenda fani hiyo sambamba na ile ya uchoraji," alisema.
Alisema alipenda sana kuchora utotoni, kipaji ambacho anaamini kama angekiendeleza angefika mbali kwa vile alikuwa mahiri kuliko maelezo.
Filamu yake ya kwanza kumtangaza mwanadada huyo ni My Book, kisha kushiriki zingine kama Saturday Morning, Better Days, Not Without My Son, Continous Love na sasa ameibuka na Second Wife.
Aisha anayependa kuogelea, kufanya mazoezi na kupika, alisema kati ya kazi zote alizoshiriki ile ya Saturday Morning ndio filamu bomba kwake kwa jinsi alivyoigiza kwa umahiri.
"Saturday Morning, ndiyo picha kali kwangu wala sio siri," alisema kisura huyo.
Akiwa na ndoto za kuja kuwa muigizaji wa kimataifa, Aisha anasema hakuna anachochukia maishani mwake kama dharau ya uongo.
"Uongo na kufanyiana dharau ni vitu nisivyopenda maishani mwangu,"
Aisha Fat'hi aliyezaliwa mwaka 1983, alisema fani ya filamu nchini inazidi kupiga hatua, ingawa alisema bado haijawa na tija ya kutosha kutokana na kuwepo kwa wizi wa wajanja wachache.
Kisura huyo ambaye waliwahi kuhusishwa na marehemu Meddy Mpakanjia, hajaolewa wala
hana mtoto na mipango yake ni kujikita zaidi katika fani hiyo ili afike mbali ikiwezekana aje kumiliki kampuni yake binafsi ya kuzalisha filamu.
"Hizi ndizo ndoto zangu, kutamba kimataifa na kuja kumiliki kampuni yangu binafsi," alisema.
Aisha, alisema kwa umri wake na kiu ya mafanikio aliyokuwa nayo naamini atafika huko
akutakapo, muhimu Mungu amjalie umri na afya njema.

No comments:

Post a Comment