STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, February 19, 2011

Nyalawila apigiwa debe, Cheka ajipanga





MAPROMOTA wa Ngumi za Kulipwa nchini, wameombwa kujitokeza kumuandalia pambano la utetezi Bingwa wa Dunia wa WBF, Karama Nyalawila, ili asipoteze taji hilo.
Rais wa Oganaizesheni ya Ngumi za Kulipwa Tanzania, TPBO, Yasin 'Ustaadh' Abdalla, alisema ili kumuepushia Nyalawila asipoteze taji lake alilotwaa mwishoni mwa mwaka jana nchini Ukraine ni vema mapromota wakajitokeza kumuandalia pambano la utetezi.
Ustaadh, alisema kwa kanuni zilizopo katika mchezo huo, bingwa yeyote akikaa muda mrefu bila kupigana, hupoteza sifa ya kushikilia taji na hivyo anahofia yasije yakamkuta Nyalawila.
"TPBO tunawaomba waratibu wa michezo ya ngumi za kulipwa nchini kumuandalia pambano Nyalawila ili kutetea taji na kuepuka kulipoteza taji hilo lenye hadhi kubwa katika mchezo huo duniani," alisema Usraadh.
Rais huyo alisema oganaizesheni yake ipo tayari kufanya kazi na promota yeyote atakayekuwa tayari kumuandalia bingwa huo wa WBF pambano hilo kwa lengo la kutaka Tanzania iendelee kung'ara kimataifa.
Alisema kwa kitambo kirefu mabondia wa Tanzania wameshindwa kung'ara kimataifa na hivyo ni vema Nyalawila, Francis Cheka na wengine wanaoshikilia mataji wakawa wanapewa kipaumbele kuandaliwa michezo.
Katika hatua nyingine, bingwa wa dunia wa WBC, UBO, ICB, Francis Cheka, anajifua kujiandaa na pambano lake la kuwania taji la IBF litakalofanyika April 2, jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na Micharazo toka Morogoro, Cheka, alisema pambano lake litafanyika kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee na atapigana na Mmarekani, Marcus Upshaw.
"Natarajia kupanda ulingoni April 2 kwa kuzichapa na Mmarekani ambaye jina lake limenitoka, katika kuwania mkanda wa IBF uzito wa kilo 72," alisema.
Hilo litakuwa pambano la kwanza kwa Cheka tangu alipomshindwa kwa pointi Bingwa wa Afrika Mashariki na Kati, Mada Maugo katika pambano lisilo la mkanda lililochezwa Januari Mosi, kwenye ukumbi wa PTA, jijini Dar.

Mwisho

No comments:

Post a Comment