STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, February 22, 2011

Msalaba Wangu upo kwa Teddy

MTUNZI anayekuja juu katika fani ya utunzi wa riwaya, Teddy Chacha, amejitosa kwenye filamu na kuibuka na kazi mpya iitwayo 'Msalaba Wangu'.
Filamu hiyo inayozungumzia masuala ya kijamii na hasa kuwepo kwa imani potofu juu ya watu wenye ulemavu, imeshirikisha 'vichwa' kadhaa nyota vya fani ya uigizaji nchini akiwemo Pembe, 'Bi Hindu' na Charles Magali 'Mzee Magali'.
Akizungumza na Micharazo, Teddy alisema filamu hiyo ni zao la moja ya hadithi zake zinazochapishwa kwenye magazeti mbalimbali likiwemo NIPASHE, ambapo inazungumzia familia moja inayomkataa mtoto wao aliyezaliwa mlemavu wa akili.
Teddy, alisema filamu hiyo ni kama simulizi la kweli kutokana na kisa alichowahi kusimuliwa na kusema ni moja ya kazi yenye kuelimisha na kuiasa jamii juu ya kuepukana na mila na desturi potofu.
"Ni moja ya kazi yenye mafunzo na hasa kutokana na wahusika kubeba uhusika wao kwa kiwango cha hali juu," alisema Teddy.
Aliongeza kuwa filamu hiyo aliyotunga na kuiongoza mwenyewe, imerekodiwa na kampuni ya Magambo Entertainment na kwa sasa inamalizwa kuhaririwa kabla ya kutafutiwa soko tayati kuwapa wadau wa filamu burudani yenye mafunzo kwao.
Teddy, aliwataja washiriki wa filamu hiyo ni pamoja na Pembe, Bi Hindu, Mzee Magali, mtoto Yasin Kamba ambaye ndiye mhusika mkuu, Mohammed Hamis, Josephine Joseph na wengine.

No comments:

Post a Comment