STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, February 28, 2011

Nyawela atuma salamu kwa wapinzani wa Extra



DANSA maarufu nchini ambaye kwa sasa ni kiongozi wa safau ya unenguaji wa bendi ya Extra Bongo, Hassan Mohammed 'Super Nyamwela', amewataka wapinzani wake kukaa chonjo na ujio wake mpya akiwa na bendi hiyo.
Nyamwela, aliyetokea African Stars 'Twanga Pepeta' amesema muda wa mwezi mmoja waliokuwa kambini amefanya mambo makubwa ambayo anaamini yatawasambaratisha wapinzani wao mara watakapotoka mafichoni.
Akizungumza mara baada ya bendi hiyo kutambulisha 'shoo' pamoja na moja ya vibao vyao vipya kwa waandishi wa habari jana, kwenye kambi yao iliyopo Mbezi-Louis jijini Dar es Salaam, Nyamwela alisema wapo kamili kwa vita.
Nyamwela alisema muda mmoja wa mwezi waliokaa kambini wameweza kuandaa shoo mpya ambazo hazijawahi kuonwa kokote.
"Kama ulivyoo, hiyo ni sehemu tu ya kazi ambazo tumekuwa tukizifanya tangu tuingie kambini na ambazo zitaanza kuonekana hadharani Ijumaa tutakapotoka mafichoni na kufanya shoo za mwishoni mwa wiki," alisema.
Alisema kikosi chao kinachoundwa na wanenguaji tisa akiwemo yeye Super Nyamwela, Super Danger, Master B na King Lion ambao ni wanaume, huku wa kike ni Angela Alloyce, Otilia Boniface, Husna Ramadhani, Lavia Edward na Jamila Nassor.
Naye rapa mpya wa bendi hiyo, Saulo John 'Ferguson' amewataka mashabiki wa muziki wa dansi kusubiri kupata vitu vipya toka kwake kuliko vile walivyokuwa wamezoea kuvipata alipokuwa Twanga Pepeta.
"Nina rapu kibao, lakini sitaki kumaliza uhondo, Ijumaa tunaanza kutoka kwa kufanya onyesho pale New Msasani Club, watu waje wamuone Ferguson mpya," alisema rapa huyo mmoja wa waimbaji wapya wa Extra Bongo.

Mwisho

No comments:

Post a Comment