STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, February 22, 2015

Simanzi! Christopher Alex hatunaye duniani!

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgTo5gnxm0hxL2vl32ZTdKTWURp8bI9AhqxaS4u79wBsu7mcRP0Bn9ulEdWLFZaFH-QzfMXd4561SJIzpTRzFR-0cOFzLUd4bEqUojYVciaPBRvmiskU_my2Mc8MEQgDkCBkGg0-aT8C85u/s1600/426453_235934163168144_100002546855024_482737_173110702_n.jpg
Christopher Alex (wa tatu toka kulia) enzi za uhai wake akiwa na kikosi kilichoing'oa Zamalek mwaka 2003
KIUNGO nyota wa zamani wa klabu ya Simba na timu ya taifa, Taifa Stars, Christopher Alex Massawe amefariki dunia asubuhi ya leo.
Kwa mujibu wa taarifa ambazo MICHARAZO imezipata mapema zinasema kuwa, kiungo huyo aliyekuwa akiugua kwa muda mrefu amefariki akiwa kalazwa katika Hospitali ya Milembe, iliyopo mkoani Morogoro.
Alex, anayekumbukwa kwa kupiga penati ya mwisho ya Simba iliyowavua ubingwa Zamalek ya Misri katika pambano la Ligi ya Mabingwa kati yao iliyochezwa mwaka 2013, alikuwa akisumbuliwa na maradhi ya kifua.
Mama mzazi wa Alex amethibitisha kutokea kwa kifo hicho ambaye alikuwa akiishi naye na kumuuguza kwa msaada wa wasamaria wema wakiwamo wadau wa soka.
Wakati klabu yake ya zamani ikiwa 'ímemsusa', mashabiki wa klabu hiyo na wengine wa soka walikuwa bega kwa bega na mama huyo kwa kuchangia fedha za matibabu, harambe kubwa ikiendeshwa na kituo cha Cloud's FM
Marehemu Christopher Alex, alizaliwa Septemba 12, 1975, na kupata elimu yake ya msingi katika shule ya msingi Uhuru na kumaliza katika shule ya Chamwino huko Dodoma mwaka 1993.
Alianza kucheza mpira kwenye timu ya daraja la nne ya Chamwino Utd na baadaye daraja la tatu akiwa na kikosi cha Aston Villa nayo ya Dodoma.

Mwaka 1999-2001, aliitumikia klabu ya CDA ya Dodoma, kabla ya kutimkia klabu ya Reli ya Morogoro mwaka 2002, na baadaye kujiunga na Wekundu wa Msimbazi Simba.
Marehemu ameacha mtoto mmoja aitwaye Alex.
MICHARAZO inatoa pole kwa ndugu, jamaa na familia nzima ya marehemu Alex kwa msiba huo na kuwaombea Subira kwa Mungu kwa kukumbuka kuwa 'Kila Nafsi Itaonja Mauti'
Mungu aiweke roho ya marehemu Alex Mahali Pema Ameen!

No comments:

Post a Comment