STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, February 22, 2015

Yanga 'watamu' kama Mcharo! Yaifumua Mbeya City

Simon Msuva aliyeanza kufungua neema ya mabao Mbeya leo
Mrisho Ngassa  akadhihrisha amerejea upya Jangwani
Amissi Tambwe akamaliza udhia kwa kufunga bao la tatu
MABAO matatu kutoka kwa Simon Msuva, Mrisho Ngassa na Amissi Tambwe yameiwezesha Yanga kupata ushindi wa pili mfululizo jijini Mbeya baada ya kuicharaza Mbeya City kwa mabao 3-1.
Mchezo huo wa Ligi Kuu Tanzania Bara ulichezwa kwenye uwanja wa Sokoine na kuiwezesha Yanga kuibuka na ushindi huo mnono ulioifanya izidi kujizatiti kileleni ikiwa na pointi 31 baada ya mechi 15.
Simon Msuva alianza kufunga katika kipindi kwanza kabla ya Ngassa 'kuzawadiwa' bao mara baada ya kipindi cha pili kutokana na mbwembwe za kipa David Burhan wa Mbeya City kumpoza.
Kipa huyo Bora wa msimu wa 2012-2013, alirudishiwa mpira na Steven Mazanda na badala ya kuupiga mbele alijaribu kumpiga chenga Ngassa aliyeunasa kilaini na kutumbukiza wavuni kaundika bao la pili la Yanga.
Amissi Tambwe aliunganisha kwa kichwa mpira wa kona uliopigwa na Haruna Niyonzima na kuiandikia bao la tatu, wakati huo tayari wenyeji alishapata bao la kufutia machozi kupitia kwa Peter Mapunda.
Bao hilo la Mapunda limeitibua rekodi ya kipa Ally Mustafa 'Barthez'ambaye alikuwa amecheza muda wa dakika 704 bila kuruhusu wavu wake kutikiswa. Dakika hizo ni 630 za mechi sita na 74 za leo kabla ya Mapunda kumtungua kufuatia mabeki wake kushindwa kuokoa.
Kwa ushindi huo Yanga imejikita kileleni ikiwa na pointi 31 baada ya mechi 15 ikijiandaa kuondoka nchini kwenda Botswana kurudiana na BDF XI katika mechi ya Kombe la Shirikisho Afrika.

No comments:

Post a Comment