STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, February 22, 2015

Liverpool yaua, Spurs, Everton zabanwa nyumbani

Hivi ndivyo vita vya Liverpool na wenyeji wao Soputhmapton ilivyokuwa Victor Wanyama akichuana na Jordan Hendeson

WAKATI klabu ya Tottenham Hotspur ikilamizika kupigana kiume kurejesha mabao mawili ili wasife nyumbani mbele ya West Ham Utd, Liverpool wameendelea kutoa dozi kwa kuicharaza Southampton kwa mabao 2-0 katika mfululzii wa Ligi Kuu ya England.
Spurs ikiwa nyumbani ilitanguliwa kufungwa mabao 2-0 kabla ya kuyarejesha baadaye na kuambulia sare ya mabao 2-2, shukrani za pekee zieende kwa Harry Kane aliyefunga bao la kusawazisha baada ya awali kukosa penati na mpira kumrudia na kuutumbukiza wavuni.
Katika mchezo mwingine timu ya mkiani ya Leicester City ilijitutumua na kulazimisha sare ya ugenini ya mabao 2-2 dhidi ya Everton kabla ya hivi punde Liverpool kuandikisha ushindi wa mabao 2-0 ugenini dhidi ya Southampton.
Mabao ya Phillipe Coutinho katika dakika ya tatu na jingine la kipindi cha pili lililofungwa na Raheem Sterling liliwapa vijogoo hao wa Anfield kupata ushindi huo uliowafanya wafikishe jumla ya pointi 45 na kulingana Spurs ingawa wameshindwa kuiengua Southampton katika nafasi ya tano wakati ligi ikiwa ipo raundi ya 26.
Katika pambano hilo wenyeji walilalamika kunyimwa penati mbili za wazi baada ya wachezaji wao kufanyiwa madhambi langoni mwa Liverpool.

No comments:

Post a Comment