STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, February 23, 2015

Mdudu wa sare ahamia Azam, yabanwa na Prisons

Azam waliolazimishwa sare isiyo na mabao na Prisons-Mbeya
MDUDU wa sare aliyekuwa ameiganda Simba, amehamia kwa mabingwa watetezi, Azam baada ya kulazimishwa sare ya kutokufungana na maafande wa Prisons-Mbeya ikiwa ni siku chache kuambulia sare nyingine kama hiyo na Ruvu Shooting Stars.
Sare hiyo ya pili mfululizzo kwa Azam imetoa nafasi kwa vinara wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga kutanua pengo lake la uongozi hadi kuwa pointi nne licha ya timu zote mbili kucheza mechi 15 kila mmoja.
Yanga inaoongoza ikiwa na pointi 31 baada ya kuvuna pointi 6 jijini Mbeya kwa kuzichapa Prisons na Mbeya City kwa mabao 3-0 na 3-1, wakati Azam kwa kupoteza pointi nne wamekusanya pointi 27.

Pambano hilo la Azam an Prisons lilichezwa usiku kwenye uwanja wa Azam Complex, Chamazi na sare hiyo isiyo na mabao imewapa afueni maafande wa Prisons waliofikisha pointi 12 baada ya kucheza mechi 15.

No comments:

Post a Comment