STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, February 23, 2015

Irene Uwoya aibarishia Kisoda kufunika 2015

https://40.media.tumblr.com/49d4dc38db37ae6d8398d8d9c5ab75c0/tumblr_n6yqbutuDQ1rtmw2wo1_500.jpg
Irene Uwoya
MSANII nyota wa filamu, Irene Uwoya, amesema kuwa anaamini filamu yake ijayo ya 'Kisoda' itakuwa funika bovu kuliko 'Apple' ambayo aliitoa mwaka mmoja uliopita.
Akizungumza na MICHARAZO, Irene anayefahamika kama 'Oprah' au Mama Krish, alisema kuwa kwa namna filamu hiyo ilivyotengenezwa kwa ubora wa hali ya juu ya kushirikisha nyota mbalimbali wa Tanzania na wale wa kimataifa ana imani ya kufunika 2015.
Irene alisema ingawa siyo vema kuanza kujisifia kabla hata filamu hiyo haijainguia sokoni, lakini anawataka mashabiki wake kuisubiri kuipokea kabla ya Pasaka kuweza kuthibitisha maelezo yake.
"Huwa sina utamaduni wa kupenda kujifagilia, lakini mashabiki wangu waisubiri 'Kisoda' waone utofauti, naamini itafunika kuliko hata 'Apple'," alisema Irene ambaye ni mmiliki wa kampuni ya Apple Film Production.
Irene alisema kuna mambo yaliyokwamisha filamu hiyo kutoka mapema kama alivyokuwa amepanga, lakini mara baada ya kuhaririwa itaachiwa na kufanyiwa uzinduzi wake kabla ya Pasaka inayotarajiwa kuadhimishwa mwanzoni mwa Aprili.

No comments:

Post a Comment