STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, February 23, 2015

Mourinho 'alianzisha' tena England, kisa sare na Burnley

http://news.bbcimg.co.uk/media/images/74475000/jpg/_74475524_74474959.jpgKOCHA Jose Mourinho wa klabu ya Chelsea, ameanzisha tena vita ya maneno na chama cha soka England, FA kufuatia kudai kuwa kampeni dhidi yake ya kuhakikisha hachukui ubingwa msimu huu inaendelea na kweli itawagharimu klabu yake.
Mourinho ameyasema hayo baada ya kutoka sare ya 1-1 na Burnley kwenye uwanja wa nyumbani wa Stamford Bridge ambapo amelaumu maamuzi ya mwamuzi Martin Alkinson.
Alkinson alimuonesha kadi nyekundu kiungo wa Chelsea, Nemanja Matic na atakosa mechi ya jumamosi ya fainali ya kombe la ligi dhidi ya Tottenham baada ya kadi nyekundu ya dakika ya 69.
Mourinho anadai Ashley Barnes alitakiwa kutolewa nje kwa kadi nyekundu kwa kumchezea vibaya Martic na kulikosababisha kiungo wake amsukume mshambuliaji huyo wa Burnley na kuambulia kadi nyekundu.
Pia alitakiwa kutolewa kwa kadi nyekundu kwa kitendo cha kumsukuma Branislav Ivanovic.
Mourinho anaamini haki haikutendeka ambapo walinyimwa penalti mbili kwani Michael Kightly aliunawa mpira wa shuti la Ivanovic katika dakika ya 33′ na nahodha wa Burnley Jason Shackell alimsukuma Diego Costa eneo la hatari dakika chache kabla ya mapumziko.
Chelsesa bao ipo kileleni mwa msimamo wa ligi ikiwa na pointi 60, wajkifuatiwa kwa mbali na Manchester City ambao walitoa kipigo cha 'Paka Mwizi' kwa Newcastle United kwa kuizabua mabao 5-0 na kufikisha pointi 55.

No comments:

Post a Comment