STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, February 23, 2015

Kocha Southampton kumuadhibu Sadio Mane, kisa...!

Southampton forward Mane battles for the ball with Liverpool midfielder Philippe Coutinho (right)
Sadio Mane akichuana na Coutinho katika mechi yao ya jana dhidi uya Liverpool na kulala nyumbani 2-0
MENEJA wa klabu ya Southampton, Ronald Koeman anakusudia kumuadhibu Sadio Mane kufuatia mshambuliaji huyo kuchelewa kufika katika mechi waliyopoteza 2-0 dhidi ya Liverpool usiku wa jana.
Mane alikuwepo katika kikosi kilichowakabili wakali wa Merseyside kwa kufika baada ya nusu saa kupita kutoka muda waliopanga kufika, saa saba mchana.
Pia mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Senegal anakabiliwa na adhabu nyingine ya kutozingatia muda.
“Alichelewa kwa dakika 25-30 kabla ya mechi”, amethibitisha Koeman.
“Tuna kanuni na maelekezo kwa wachezaji. Kila mtu anaweza kuchelewa siku moja asubuhi, lakini huwezi kuchelewa kufika saa saba wakati unacheza dhidi ya Liverpool.
“Hakutoa maelezo? Maelezo hayo ni baina ya kocha na mchezaji, lakini alichelewa.
‘Siwezi na sikubaliani na hilo. Kama ni kulipa faini alipe tu”

No comments:

Post a Comment