STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, February 23, 2015

Mwili wa Mez B kuzikwa leo mjini Dodoma

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEimP0azU_N4UKy6iarXropB_bWlOXWyV6TN5j6W57e0WoMdC59awKdXuKv1AnvZJsNTfAnaLl4hqWKSUST5yF0bw1uTgBWXiPY-qT4tXAdnHOjdm9QuoqHdYBs2IVm5TJMJYuzSB7BZJzk/s1600/Mez-B1.jpg 
http://laurent.antibi.perso.sfr.fr/WEBSITE/SiteV2/Mez%20B%20-%20Kama%20Vipi.jpg 
MWILI wa msanii nyota wa muziki wa kizazi kipya, Moses Bushagama maarufu kama Mez B aliyefariki dunia Ijumaa iliyopita wakati akikimbizwa hospitalini unatarajiwa kuzikwa leo katika Makaburi ya Wahanga wa Treni yaliyopo Mailimbili  mjini Dodoma.
Taarifa iliyotolewa na mama yake  Mez B, Merry Katambi alisema  shughuli ya kumuaga mwanae itafanyika Viwanja vya Nyerere Square Mjini hapa.
Mazishi hayo kwenye viwanja vya Nyerere yataambatana na ibada ya kumuombea na yanatarajiwa kuanza saa saba mchana.
"Mwanangu tutamzika Jumatatu (leo) katika Makaburi ya wahanga wa Treni Mailimbili ila ibada pamoja na kuuga mwili wa marehemu zitafanyika katika viwanja vya Mwalimu Nyerere’’ 
Mez B alikuwa ni mwanzilishi wa kundi la Chemba Squard ambapo alikuwa pamoja na Dar Master, Noorah na Albert Mangwea huku akitamba na nyimbo za 'Kikuku cha Mama Rhoda', 'Nimekubali' na 'Kama Vipi iliyomjengea jina kubwa kwa mashabiki wa muziki kabla ya 'kuzimika'.

No comments:

Post a Comment