STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, February 23, 2015

Twiga Stars waingia kambini kujiwinda kimataifa

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiAZV4PJLK51AfIOWLOo-LS5q0FtMrlxask2Emm9hlzaIXdFSfvk8D33r9A9WSNUG4UKAQzsdUe81YTuke-D4AvaFFQMl-HBoHd_nOp0iXI0NJsfzUIYWQH-LL_wbKgMm7NLqRX0BLqbOQ/s1600/KAIJAGE.JPG
Kocha wa Twiga Stars
http://api.ning.com/files/STHDuz-8NrUpchIxJtAG7Yhc*bs7v9f6guq0lMwxNXrwwbY8mQyceglvUwtFfk9Y9Lg8A7-*-yAlwpgOnTx01kmvHI749vQs/TWIGA.JPG
Baadhi ya nyota wa Twiga Stars walioitwa kambini
KIKOSI cha wachezaji 30 kilichoitwa na Kocha Mkuu wa timu ya Taifa ya Wanawake Tanzania (Twiga Stars), Rogasian Kaijage kimeingia kambini tayari kwa maandalizi ya mchezo wa kufuzu Fainali za Mataifa Afrika dhidi ya Zambia utakaodfanyika mwezi ujao.
Kaijage ametangaza programu yake ya  mazoezi itakayochukua takribani wiki nne (4) ili kuhakikisha wachezaji wanakua tayari kwa ajili ya mchezo huo utakaochezwa kati ya Machi 21, 22 mwaka huu, huku akipanga kucheza mchezo mmoja wa kirafiki kabla ya kuelekea Lusaka Zambia kwenye mchezo wa awali.
Twiga Stars ambayo imeingia kambini jana Jumapili na itakuwa kwenye Hosteli za Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini TFF zilizopo Karume,  imefuzu moja kwa moja katika hatua ya pili kucheza na Zambia kufuatia kuwa na matokeo mazuri katika msimamo wa viwango vya soka la wanawake barani Afrika.
Wachezaji walioitwa na kuingia kambini ni pamoja na Asha Rashid 'Mwalala', Esther Chaburuma 'Lunyamila', Fatuma Bushiri, Fatuma Hassan, Fatuma Mustapha, Fatuma Omari, Eto Mlenzi, Mwajuma Abdallah, Sofia mwasikili, Zena Khamis, Mwanahamis Omar, Fatuma Khatibu, Fadhira Hamad, Anastazia Anthony, Shelder Boniface.
Wengine ni Thereza Yonna, Happines Hezron, Amina Ally, Donizia Daniel, Fatuma Issa, Vumilia Maarifa, Maimuna Hamisi, Najiati Abbasi, Stumai Abdallah, Ziada Ramadhani, Zuwena Aziz, Irene Joseph, Dawa Haji Vuai, Belina Julius na Amina Ramadhani.

No comments:

Post a Comment