STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, February 22, 2015

Mnyama afa Shinyanga, Stand Utd yaifanyizia

Kikosi cha Simba
BAADA ya kufanikiwa kuondoa 'gundu' kwa Polisi Moro na kudai walikuwa wameianza rasmia Ligi Kuu, klabu ya Simba leo ametolewa nishai ugenini mjini Shinyanga kwa kukubali kipigo cha bao 1-0.
Kipigo hicho kimetolewa kwa Simba na timu ya Stand United katika pambano tamu lililochezwa kwenyue uwanja wa Kambarage na kuzima mbwembwe za vijana wa Msimbazi huku mashabiki wao wakiibua zogo.
Zogo hilo lililosababisha pambano hilo kusimama kwa muda ilitokana na imani kwamba lango la wapinzani wao lilikuwa limefukiwa 'vitu' ambavyo vilikuwa vikiwafanya vijana wao kushindwa kufunga mabao.
Bao pekee lililowaua Simba ya kocha Goran Kopunovic, liliwekwa kimiani na Mnigeria Absalim Chiibibele likiwa ni bao lake la tano msimu huu katika dakika ya 11 na kuwafanya Simba kuhaha kurirejesha bila mafanikio.
Kwa kipigo hicho Simba imesaliwa na pointi pointi 20 baada ya mechi 16 wakati Stand imefikisha pointi 18 baada ya mechi 16 pia na itavaana na Kagera Sugar katika mechi yao ijayo mjini Shinyanga.

No comments:

Post a Comment