STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, December 23, 2014

Salha Abdallah adai alili-miss Jukwaa

Salha katika pozi
Salha wa Hammer
MUIMBAJI mpya wa kundi la muziki wa taarab la Five Star, Salha Abdallah 'Salha wa Hammer' amesema kurejea kwake jukwaani kumemfanya kujisikia faraja kubwa kwa vile 'alilimisi' jukwaa hilo kwa muda mrefu.
Salha aliyekuwa akiliimbia kundi la King's Modern 'Wana Zima Taa', alikuwa kwenye likizo ya uzazi jambo lililomfanya asionekane jukwani kwa zaidi ya miezi minne na hivi karibuni alijiunga na kundi la Five Star lililozindua albamu yao mpya ya 'Kichambo Kinakuhusu' akiwa miongoni mwa waimbaji wa nyimbo za albamu hiyo.
"Kwa kweli 'nililimisi' sana jukwaa, nimejisikia faraja kurudi tena ulingoni. Naamini baada ya 'Kishtobe cha Mtaa' kuna kazi nyingine kali zaidi zinakuja," alisema Salha.
'Kishtobe cha Mtaa' ni wimbo alioimba mwanadada huyo ambaye ni mke wa muimbaji mwingine nyota wa miondoko ya taarab na mduara, Hammer Q.
Salha alisema mashabiki waliomkosa kwa muda mrefu ni fursa yao ya kujitokeza kwenye maonyesho ya kundi lake jipya kupata burudani.

No comments:

Post a Comment