STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, December 23, 2014

Muhammad Ali anaendelea vyema hospitalini

http://worldsportss.com/wp-content/uploads/2014/10/Muhammad-Ali-101.jpgHALI ya Bingwa wa zamani wa Masumbwi Duniani kwa Uzani wa Juu, Muhammad Ali inaendelea vyema.
Msemaji wa gwiji huyo aliyekimbizwa hospitalini mwishoni mwa wiki kutokana na maradhi ya maambukizi katika mapafu, alisema Ali anaendelea vema. 
Msemaji huyo, Bob Gunnell amesema madaktari wanaomtibu Ali wana matumaini ya kumruhusu katika kipindi cha karibuni. 
Gunnell aliendelea kudai kuwa familia ya nguli huyo bado inaomba suala hilo kuachwa kuwa la binafsi na kushukuru maombi yote ya kumtakia heri. 
Ali, 72, bingwa wa wa zamani mara tatu wa uzito wa juu duniani ambaye anaugua ugonjwa wa kutetemeka au Parkinson alikimbizwa hospitali Jumamosi iliyopita. Ali aligundulika kuwa na Parkinson mwaka 1984, miaka mitatu baada ya kutangaza kustaafu masumbwi.

No comments:

Post a Comment