STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, December 23, 2014

Chelsea haishikiki England, yainyoa Stoke City kwao x2



Diego Costa akitafuta bao langoni mwa wenyeji Stoke City

Costa akichuana na wachezaji wa Stoke City

Cesc Fabregas akishangalia bao lake
MABAO mawili yaliyowekwa kimiani katika kila kipindi kimeiwezesha Chelsea kupata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Stoke City na kwenda kula sikukuu ya Krismasi ikiwa kileleni kwa mara ya nne sasa.
Vijana Jose Mourinho wakiokuwa ugenini katika uwanja wa Britania, walipata ushindi huo uliowafanya wazidi kujikita kileleni mwa msimamo wakiwa na pointi 42, tatu zaidi ya walizonazo mabingwa watetezi ambao waliwakamata Jumamosi baada ya kuizabua Crystal Palace mabao 3-0.
Nahodha John Terry aliiandikia Chelsea bao la kuongoza dakika mbili tu baada ya kuanza kwa mchezo huo akiunganisha mpira wa kona na kiungo nyota wa Hispania ambaye anaongoza kwa kutengeneza mabao 12 mpaka sasa ndani ya Chelsea aliiandika bao la pili dakika ya 78 kabla ya kumalizika kwa pambano hilo.
Ligi hiyo inatarajiwa kuendelea tena siku ya Ijumaa ambayo itakuwa Boxing Day kwa vinara hao kushuka dimbani kuumana na West Ham United kwenye uwanja wa Stanford Bridge.
Mechi nyingine siku hiyo ni kama zifuatavyo:
Burnley v  Liverpool Crystal Palace  v Southampton  
Everton v Stoke City
Leicester City v  Tottenham Hotspur
Manchester United  v  Newcastle United 
Sunderland   v   Hull City       
Swansea City  v   Aston Villa 
West Bromwich Albion v  Manchester City
Arsenal  v  Queens Park Rangers

No comments:

Post a Comment