STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, December 22, 2014

Tanzania yaongeza idadi ya waamuzi wa FIFA

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEifK0Ir0eMKHnBlb0rlOEKXM0IzeBuyw_3cgWPyRyAnzQLjK1RFMKyti6j2Mj_dIj4s0X3dXHRq0UuFIJRbA4gMuAGimsyjPYjL8bgDB16zX2azcV47vpbT2aiaWgfNZlTMgYeXZ7Y-nk3D/s1600/DSC_0823.jpg
SHIRIKISHO la soka Duniani, FIFA limetoa orodha mpya ya waamuzi linaowatambua ambapo katika orodha hiyo kuna jumla ya marefa 18 wa Tanzania, miongoni mwao 11 ni wapya na saba wa zamani. 
Waamuzi wapya wa kati kutoka Tanzania ni Mfaume Ali Nassor kutoka Zanzibar pamoja na Martin Saanya kutoka Morogoro.
Pia wamo waamuzi watatu wa kike ambao ni Florentina Zabron, Jonesia Rukyaa pamoja na Sofia Ismail. 
Kwa upande wa waamuzi wasaidizi wanaume ni Frank John Komba na Soud Idd Lila, kwa upande wa wanawake ni Kudura Omary Maurice, Hellen Joseph Mduma, Dalila Jafari Mtwana na Grace Mawala. Waamuzi wa zamani wa Tanzania kwenye orodha ya FIFA, kwa upande wa wanaume ni Israel Mujuni Nkongo na Waziri Sheha Waziri, kwa upande wa waamuzi wasaidizi ni Josephat Bulali, Fernand Chacha, John Longino Kanyenye, Ali Kinduli na Samuel Hudson Mpenzu.

No comments:

Post a Comment