STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, December 23, 2014

Newz Alert! Simba yapata pigo Zenji wakiiwinda Kagera Sugar

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhrM2-h9AiqcqsrWvWx9Jx0JTltliwtnjqzkQ-O2YA5w54Gyk592pkskTvj6KPw09h0s8OSRGPQmfqtbaw9apfIAYHhhHGH9QFdR9kBYCH7nCtKpa10ZmrCRGaZMycXiFOwAfZuLmm5hbE/s1600/DSC_0919.JPG
Elias 'Magoli' Maguli (kushoto)
WAKATI wakiwa katika maandalizi ya 'kuiua' Kagera Sugar katika mechi yao ya Ligi Kuu Tanzania itakayochezwa siku ya Ijumaa, Simba imepata pigo katika kambi yake visiwani Zanzibar baada ya mshambuliaji wake nyota Elias 'Magoli' Maguli kuumia kifundo cha mguu.
Simba ambao wamekimbilia Zenji siku ya Jumapili kwa ajili ya kujaindaa na pambano hilo dhidi ya Kagera litakalochezwa kwenye uwanja wa Taifa, itamkosa Maguli katika pambano hilo kwa kuapata majeraha.

Maguli ambaye aliitungua Yanga wakati timu yake wakiizamisha kwa mabao 2-0 kwenye pambano la Nani Mtani Jembe-2 lililochezwa Desemba 13, aliumia kifundo hicho wakati wa mazoezi na hivyo kumweka nje ya dimba mpaka apone.
Kukosekana kwa Maguli, mmoja wa wachezaji wenye vipaji na nguvu kubwa awapo uwanjani ni mtihani kwa Simba ambayo inakabiliana na timu ngumu inayonolewa na kocha Mganda Jackson Mayanja ambao mara kadhaa wamekuwa wakiisumbua timu hiyo kwenye uwanja huo wa Taifa.
Pia Simba ipo katika hati hati ya kupata huduma za nyota wake wa Kiganda, Emmanuel Okwi ambaye yupo nchini kwao kwa ajili ya maandalizi ya kufunga ndoa.
Ligi Kuu Tanzania Bara iliyokuwa imepumzika tangu NOvemba 9 itaendelea tena Ijumaa kwa pambano moja kati ya Simba na Kagera Sugar na kuendelea siku zinazofuaata kwa michezo kama ifuatavyo:
JUMAMOSI:
Mtibwa Sugar vs Stand United
Prisons-Mbeya vs Coastal Union
JKT Ruvu vs Ruvu Shooting

JUMAPILI:
Mbeya City vs Ndanda Fc
Polisi Moro vs Mgambo JKT
Yanga vs Azam

No comments:

Post a Comment