STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, October 18, 2014

Bayern yazidi kuchinja Bundesliga yapiga mtu 6-0

Mario GotzeMABINGWA watetezi wa Ligi Kuu ya Ujerumani, Bayern MUnich wamezidi kuimarisha uongozi wao kwa kuibamiza bila huruma Werder Bremen kwa mabao 6-0.
Phillip Lahm na Mario Gotze walifunga mara mbili, huku Xabi Alonso na  Thomas Muller wakimalizia udhia kwa kuwekwa mingine kimiani na kuifanya vijana wa Pep Guardiola kufikisha pointi 20 baada ya michezo nane ya ligi hiyo maarufu kama Bundesliga.
Katika mechi nyingine za ligi hiyo Mainz 05 ikiwa nyumbani iliitambia     Augsburg kwa mabao 2-1, Hannover 96 ikalala nyumbani kwa mabao 3-0 dhidi ya Borussia Mönchengladbach, huku Freiburg  nao wakilala nyumbani 2-1 kwa Wolfsburg.
Timu za  Stuttgart na Bayer Leverkusen zilitoshana nguvu kwa kufungana mabao 3-3, huku FC Koln ikishinda nyumbani 2-1 dhidi ya Borussia Dortmund na hivi punde Schalke 04 ikiwa nyumbani iliitambia Hertha Berlin kwa mabao 2-0.

No comments:

Post a Comment