STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, March 18, 2014

Chelsea kuifuta machozi England leo Ligi ya Mabingwa Ulaya?

CHELSEA leo inatarajiwa kuvaana na Galatasaray, ambapo mashabiki wa England wanataka kuona kama watawafuta machozi baada ya timu zao mbili za Arsenal na Manchester City ziking'olewa kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Timu nyingine ya England itakayoshuka dimbani kesho ni Manchester Unitd ambayo imewakatisha tamaa mashabiki wao kwa mwenendo wao mbaya na hivyo kutokuwa na tumaini nao kama watavuka 16 Bora na kuingia Robo fainali dhidi ya Olympiacos ya Ugiriki waliowanyoa 2-0 ugenini wiki mbili zilizopita.
Chelsea iliyoambulia sare ya 1-1 inavana na Gala, huku mshambuliaji wake wa zamani Didier Drogba hajui ni kwa namna gani ataweza kucheza kwa hamasa kubwa katika Uwanja wa Stamford Bridge  katika mechi hiyo ya leo.
Drogba alitwaa ubingwa wa England mara tatu, Kombe la FA mara nne, Kombe la Ligi mara mbili na ubingwa ulioweka kumbukumbu Ligi ya Mabingwa Ulaya 2012 akifunga penalti ya mwisho akiwa na Chelsea kwenye mechi ya fainali dhidi ya Bayern Munich katika Uwanja wa Allianz Arena.
Alifunga mabao 157 katika mechi 341 alizoichezea Chelsea kati ya 2004-12 huku akichaguliwa kama mchezaji wa kiwango cha juu zaidi katika historia ya klabu hiyo.
"Ni klabu ambayo nimepata uzoefu wa kila kitu," Drogba aliiambia tovuti ya UEFA (www.uefa.com). "Nimepata uzoefu wa kiwango cha juu, mechi kubwa na imenipa fursa ya kuwa karibu na wachezaji bora duniani.
"Ni kipindi maalumu kwangu kwa sababu sijui ni kwa vipi morali wangu utakuwa. Ninakubaliana kabisa kuhusu hili," alisema jijini Istanbul baada ya kutoka sare ya 1-1 na Chelsea.
Jose Mourinho alionekana akikaribia kumwaga chozi baada ya kupewa mapokezi mazuri katika awamu yake ya pili Stamford Bridge mwanzoni mwa msimu lakini anaamini Drogba anastahili heshima zaidi kutoka kwa mashabiki.
"Nadhani ninaruhusiwa kusema kwamba nitapata mapokezi mazuri kwa sababu ninajua mashabiki wa Chelsea na uhusiano wetu ulivyo wa kipekee," alisema Drogba.
"Itakuwa ni vizuri kuwaona kwa mara nyingine. Ninamtazamo wa mbeleni katika hilo."
Mourinho alimnunua Drogba na kumpeleka Stamford Bridge akitokea Olympique Marseille ambapo waliweza kushirikiana vema katika kufanya makubwa.
"Wakati Chelsea ikifikiria kunisajili, alikuwa ni Mourinho ambaye alikuja kuniona," alisema mchezaji huyo (36)- "Alisema, 'kama unataka kuwa mshmbuliaji mkubwa kama Thierry Henry ama Ruud van Nistelrooy, unapaswa kuja na kucheza chini yangu.
"Ni kweli nilikuwa mchezaji mzuri nikiwa Ligi ya Ufaransa lakini alinifanya kuwa mmoja kati ya wachezaji bora Ulaya. Ndiyo maana mimi, kwa Jose tunaweza kwenda sambamba hadi mwisho wa dunia.
Miamba hiyo ya Uturuki ni timu inayokuja kwa kasi, hivyo Chelsea itahitaji kufuta makosa yake baada ya Jumamosi kuangukia kichapo dhidi ya Aston Villa.
Ronaldo kuendelea kuweka rekodi Ulaya leo?
Katika mechi nyingine ya leo vinara wa Hispania, Real Madrid,  itakuwa inakamilisha ratiba yake ya kusonga mbele dhidi ya Schalke 04 baada ya mechi ya awali kuibuka na ushindi wa mabao 6-1 ugenini.
Katika mechi ya leo Real inatarajia kumpa nafasi Isco kuonyesha thamani yake baada ya kushindwa kupata namba ya kudumu chini ya Carlo Ancelotti tangu alipojiunga na timu hiyo kwa fungu kubwa akitokea Malaga.
Isco alikuwa ni biashara kubwa sokoni msimu uliopita baada ya kuiwezesha Malaga kutinga hatua ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Hata hivyo, Ancelotti anaamini bado Isco anaweza kuzoea nafasi mpya anayochezeshwa, kama ilivyokuwa kwa Mholanzi Clarence Seedorf.
"Anahamasisha kupata namba ya kuanza kikosi cha kwanza. Kwa sasa ninamuamini. Mwanzoni alikuwa kama ilivyokuwa kwa Seedorf ambaye baadaye alipata uzoefu na kuwa mchezaji muhimu kwa Milan," Ancelotti alisema mapema mwezi huu.
Kivumbi kingine cha ligi hiyio kuhitimisha timu mbili za mwisho za kutiunga robo fainali zitachezwa kesho kwa mechi kati ya Manchester United itakuwa nyumbani kuikaribisha Olympiakos Piraeus kwenye Uwanja wa Old Trafford, ikiwa inaugulia kipigo cha mabao 3-0 ilichopewa wikiendi na Liverpool.
Pambano jingine litakuwa kati ya wanafainali wa mwaka jana, Borussia Dortmund itakuwa nyumbani nchini Ujerumani kuivaa Zenit St Petersburg waliowanyonyoa kwao mabao 2-0.
Timu za Bayern Munich ya Ujerumani, Barcelona ya Hispania, PSG ya Ufaransa na Atletico Madridi zenyewe tayari zimetangulia hatua hiyo baada ya kiushinda mechi zao wiki iliyopita.

No comments:

Post a Comment