STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, March 7, 2015

Spurs yailipua QPR kwao yaipumulia Liverpool

.
Muunganiko wa picha zilizochapishwa na Daily Mail zikionyesha mpambano wa Spurs na QPR ulivyokuwa leo
MSHAMBULIAJI Harry Kane amefunga mabao mawili jioni ya leo na kuiwezesha timu yake ya Tottenham Hotspur kupata ushindi muhimu ugenini dhidi ya QPR katika mechi ya kiporo cha Ligi Kuu ya England.
Kane ambaye amekuwa moto wa kuotea mbali alifunga mabao hayo katika kila kipindi na kuifanya Spurs kufikisha pointi 50 na kupaa hadi nafasi ya sita nyuma ya Liverpool iliwatanguliwa kwa pointi 51.
Mshambuliaji huyo kinda alifunga bao la kwanza dakika ya 34 kabla ya kuongeza la pili dakika ya 68 na wenyeji wanaopambana kuepuka kushuka daraja ilip[ata bao la kufutia machozi kupitia Sandro katika dakika ya 75.

No comments:

Post a Comment