STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, March 9, 2015

AIBU! Mtoto mwingine albino akatwa kiganja Rukwa

http://ak2.picdn.net/shutterstock/videos/3573986/preview/stock-footage-close-up-of-bloody-knife-with-blood-dripping.jpg 
MATUKIO ya Ukatili dhidi ya albino yanaendelea kuwa tishio nchini Tanzania baada ya mtoto wa miaka sita kukatwa kiganja cha mkono.
Shambulio hilop jipya limetokea mkoani Rukwa kusini magharibi mwa nchi hiyo.
Mtoto huyo kiume Baraka Cosmas alikuwa amelala na mama yake mzazi wakati wahalifu hao walipovamia nyumba yao.
Kamanda wa polisi Mkoa wa Rukwa Jackob Mwaruanda amesema kwa sasa mtoto huyo anapata matibabu hospitali na hali yake inaendelea vizuri.
Polisi inaendelea na uchunguzi kubaini wahusika.
Shambulio hilo linajitokeza wiki moja tu baada ya watuhumiwa wanne kuhukumiwa adhabu ya kifo kwa mauaji ya albino.
Pia ni muda mfupi baada ya Rais Tanzania Jakaya Kikwete kukemea mauaji ya albino, ambao viungo vyao hutumika katika shughuli za kishirikina kwa imani potofu kuwa zinasaidia kuleta utajiri na madaraka.
Kadhalika kukiwa kumeanzishwa kampeni maalum ya 'Inatosha' kukomesha mauaji hayo ya albino ambayo yameitia aibu Tanzania katika usoa wa dunia.

No comments:

Post a Comment