STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, August 27, 2011

Wasomi CCM, wamlilia Kikwete avunje ukimya kwa yanayoendelea nchini



RAIS wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzaania, Dk Jakaya Kikwete ametakiwa kutekeleza kwa vitendo dhana ya uwajibikaji kwa kuwatimua kazi mawaziri ambao wizara zao zimekumbwa na kashfa ikiwemo wa Nishari na Madini na ile ya Maliasili na Utalii.
Aidha serikali imeombwa kuchukua hatua ya haraka katika kutatua matatizo yaliyopo katika sekta ya elimu ikiwemo suala la kutimuliwa kwa wahadhiri na kusimamishwa kwa wanafunzi wa vyuo vikuu vya Dodoma, UDOM, taasisi ya IMTU na Chuo cha Ustawi wa Jamii.
Wito huo umetolewa na Shirikisho la Wana-CCM Vyuo vya Elimu ya Juu mkoa wa Dar es Salaam, katika mkutano wa viongozi wake na waandishi wa habari uliofanyika juzi jijini humo.
Mwenyekiti wa Shirikisho hilo, Lusekelo Mwandemange, alisema bila Rais Kikwete kufanya maamuzi magumu katika utekelezaji wa vitendo dhana ya uwajibikaji ni wazi serikali yake itaendelea kupoteza sifa mbele ya wananchi.
Mwandemange alisema kwa kuwa dhana ya uwajibikaji ipo ndani ya CCM tangu enzi za Hayati Baba wa Taifa, Mwl Nyerere, katika kulinda maadili ya viongozi ni vema Rais Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM Taifa akatekeleza kwa kuwawajibisha baadhi ya watendaji wake.
Mwenyekiti huyo alisema kwa kashfa zilizoikumba wizara za Nishati na Madini na ya Maliasili na Utalii za kusimamishwa baadhi ya watendaji wake haipaswi kuachwa kwa wahusika tu bila mawaziri wanaoziongoza wizara hizo kuwajibishwa kwa yaliyotokea.
Mwandemange alisema ni vigumu wananchi kuielewa serikali kama watu waliovurunda mambo serikalini wakapewa likizo za malipo na kurejeshwa kinyemela kwa bashasha kama mashujaa, wakati wanafunzi wanaosimama kutetea haki zao wakitimuliwa vyuoni bila huruma yoyote.
"Tunamuomba Mwenyekiti wetu wa CCM ambaye ndiye Rais wa Jamhuri, afumbe macho na kuwapiga chini (kuwaondoa) viongozi wote dhaifu serikalini, bila kufanya hivyo hatutaweza kurudisha taswira nzuri ya serikali na chama mbela ya wananchi," alisema Mwandemange.
Aliongeza pia kwa kulipongeza Bunge la Jamhuri kwa uamuzi wa kuunda Tume ya

kuchunguza upya sakata la katibu wa wizara ya Nishati na Madini, akiiomba Tume hiyo isiishie kwa David Jairo, bali iimulike wizara nzima pamoja na wizara nyingine za serikali zilivurunda.
"Tume hiyo ichunguze kashfa ya wizara ya Maliasili na Utalii ambayo waziri wake, Ezekiel Maige aliwasimamisha watendaji wake akiwemo Mkurugenzi wa Idara ya Wanyama Pori nchini, Obed Mbangwa bila mwenyewe kuwajibika kwa hilo," alisema.
"Kwa hili tunashangaa waziri anaendelea kukalia kiti kwa kuwasimamisha kazi watendaji wake kwa staili ile ile ya Jairo, alikuwa wapi siku zote hadi wabunge walipofichua, lazima naye awajibike, ndio maaana tunamkata Rais avunje ukimya kwa kuwajibisha wahusika," aliongeza.
Shirikisho hilo liligusia matatizo ya sekta ya elimu yaliyopo katika baadhi ya vyuo vikuu nchini kwa kuitaka serikali ichukue hatua za haraka kuyatatua, licha ya kuipongeza kwa uamuzi wa kuongeza posho za wanavyuo kutoka Sh 5,000 hadi kuwa Sh 7,000.
Uongozi wa shirikisho hilo kupiotia taarifa yao iliyosainiwa na Katibu Mkuu wao, Asenga Abubakar, umesema hawakubaliani na maamuzi ya fedha za mikopo kupelekwa moja kwa moja vyuoni badala ya Bodi ya Mikopo kama zamani wakidai itazidisha matatizo.
Pia waliiomba serikali kuwarejesha wanafunzi na wahadhiri walitimuliwa na kusimamishwa vyuo vya Chuo cha Ustawi wa Jamii, taasisi ya IMTU na UDOM, wakidai kinachofanywa dhidi yao ni uonevu aliodai kama shirikisho hawaridhiki nayo.

No comments:

Post a Comment