STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, December 21, 2014

Raheem Sterling atwaa tuzo akiisubiri kwa hamu Arsenal leo

http://assets.lfcimages.com/uploads/9559__1458__sterling560_512X287.jpg
Raheem Sterling akiwa na tuzo yake
http://i1.liverpoolecho.co.uk/incoming/article8287825.ece/alternates/s1023/JS52985656.jpg
Sterling akiwajibika uwanjani

WAKATI leo akitarajiwa kuiongoza klabu yake ya Liverpool watakapoikaribisha Arsenal, Raheem Sterling amefanikiwa kushinda tuzo ya Golden Boy kwa mwaka huu na kuwa Mwingereza wa kwanza kushinda tuzo hiyo toka Wayne Rooney aliposhinda mwaka 2004. Msghambuliaji huyo nyota wa Liverpool ametwaa tuzo hiyo kwa umahiri wake uliomfanya kuwa mchezaji muhimu katika kikosi cha Liverpool huku akiwa amejihakikishia namba katika kikosi cha timu ya taifa. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 20, amewashinda chipukizi wenzake akiwemo Adnan Januzaj wa Manchester United na Hakan Calhanoglu wa Bayer Leverkusen pamoja an wachezaji wenzake wa Liverpool Lazar Markovic na Divock Origi. 
Akihojiwa Sterling aliuambia mtandao wa Liverpool kuwa ni mafanikio makubwa kushinda tuzo kama hiyo na ni jambo la furaha kwake na familia yake. Wachezaji wengine wlaiowahi kushinda tuzo hiyo ni pamoja na Lionel Messi, Cesc Fabregas na Sergio Aguero.
Mshambuliaji huyo leo anatarajiwa kuingoza timu yake kuikaribisha Arsenal kwenye uwanja wa Anfield katika mechi ya Ligi Kuu ya England linalosubiriwa kwa hamu.
Katika mechi kama hiyo katika msimu uliopita, Raheem akisaidiana na nyota wenzake Martin Skrtel na Daniel Sturridge waliiangamiza Arsenal kwa mabao 5-1.
Raheem katika mchezo huo alifunga mabao mawili sawa na Skrtel na jingine liliwekwa kimiani na Sturridge ambaye bahati mbaya leo hatakuwepo dimbani kutokana na kuwa majeruhi.
Pia mchezaji aliyechangia ushindi huo Luis Suarez hayupo kikosini kwa vile amehamia Barcelona hali na kwa mwenendo iliyonayo timu hiyo msimu huu inaleta mashaka kama wanaweza kurudia ilichofanya msimu uliopita.

M

No comments:

Post a Comment