STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, December 21, 2014

Real Madrid bingwa wa Dunia, Aucland City waitoa nishai Cruz Azul

Bale akilibuzu kombe la Klabu Bingwa la Dunia baada ya jana kuiwezesha Real Madird kulitwaa kwa kuinyuka San Lorenzo
Wachezaji wa Real madrir wakiwa na taji la Klabu Bingwa la Dunia
Wachezaji wa Real Madrid wakishangilia taji lao
Real Madrid star Cristiano Ronaldo kisses the Club World Cup trophy after their triumph
Ronaldo akilibusu taji
MABINGWA wa Ulaya, Real madrid wameliwekwa kibindoni taji la kwanza la Klabu Bingwa ya Dunia na kuwa taji la nne katika mwaka 2014 baada ya kuinyuka San Lorenzo ya Amerika Kusini kwa mabao 2-0.
Madrid iliinyoa Mabingwa hao wa Amerika Kusini katika panbano la fainali ya michuano hiyo ya Klabu Bingwa Duniani lililochezwa usiku wa jana mjini Marrakech, Morocco ikiwa ni baada ya miaka 12 tangu klabu hiyo iliposhiriki michuano hiyo.
Mabao ya beki Sergio Ramos katika dakika ya 37 na jingine na winga na mchezaji ghali duniani, Gareth Bale katika dakika ya 51 yalitosha kuwapa Real Madrid taji hilo la kwanza kwao na kuendeleza reklodi ya kucheza mechi 22 bila kupoteza msimu huu.
Katika mechi nyingine ya kusaka mshindi wa tatu wa michuano hiyo timu ya Aucland City ya New Zealand ilifanikiwa kutwaa ushindi wa tatu baada ya kuinyuka Cruz Azul ya Mexico kwa mikwaju ya penati 4-2.
Awali timu hizo zilizomaliza muda wa kawaida wa dakika 90 na ule wa nyongeza wa 120 kwa kufungana bao 1-1, Wamexico wakilazimika kusawazisha baada ya kutanguliwa na wapinzani wao ambao waliong'olewa hatua ya Nusu fainali za San LOrenzo.

No comments:

Post a Comment