STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, December 21, 2014

Southampton yazinduka, Spurs kanyaga twende England

Southampton
Southampton wakiangika moja ya mabao yao
Graziano Pelle
Pelle akimtungua Tim Howard
Erik Lamela, Tottenham
Spurs wakiangilia moja ya mabao yao mawili walipoizamisha Burnley
BAADA ya kufungwa mechi tano mfululizo zikiwamo nne za Ligi Kuu na moja ya Kombe la Ligi, hatimaye Southampton wikiendi hii imezinduka baada ya kuinyoa Everton mabao 3-0 na kuendelea kusalia kwenye nafasi ya tano katika msimamo wa ligi hiyo inayoongozwa na Chelsea.
Bao la penati la Romeo Lukaku katika dakika ya 38 na mengine mawili ya kipindi cha pili kupitia kwaGraziano Pelle katika dakika ya 65 na lile la Maya Yoshida dakika nane kabla ya kumalizika kwa pambano kuliwafanya Southampton kuonja ushindi ikiwa nyumbani na kufikisha pointi 29.
Katika mechi nyingine za ligi hiyo Mashetani Wekundu wakiwa ugenini walishindwa kuitambia Aston Villa waliokuwa pungufu kw akutoka sare ya 1-1, Mabingwa watetezi, Manchester City wakipata ushindi wa nyumbani wa mabao 3-0 dhidi ya Crystal Palace na Tottenham Hotspur ikiwa nyumbani White Hartlane waliishinda timu ya Burnley mabao 2-2 na kuwaengua Arsenal waliokuwa juu yao.
Pia timu ya QPR ikiwa nyumbani iliwaduwaza wageni wao West Bromwich kwa kuwalaza mabao 3-2, Hull City ikakubali kipigo cha nyumbani cha bao 1-0 dhidi ya Swansea City na West Ham United ikatamba nyumbani dhidi ya Leicester City kwa kuilaza mabaio 2-0.
Ligi hiyo itaendelea leo kwa michezo miwili, Liverpool itaialika Arsenal uwanja wa Anfield na wapinzani wajadi Newcastle United itaonyeshana kazi na Sunderland katika mchezo mwingine kabla ya kesho kushuhudiwa vinara Chelsea wakikwaruzana na Stoke City ugenini.

No comments:

Post a Comment