STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, December 21, 2014

Muhammad Ali akimbizwa hospitalini

http://media.washtimes.com/media/image/2012/09/13/people-muhammad-ali_lea.jpg
Bingwa wa zamani wa Dunia, Muhammad Ali
 BINGWA wa zamani wa Dunia wa Ngumi za Kulipwa Uzito wa Juu, Muhammad Ali, amekimbizwa hopitalini baada ya kubanwa na 'Vichomi' (Pneumonia)
Mwanamasumbwi hiuyo aliyenyakua ubingwa huo wa dunia mara tatu kwa mujibu wa msemaji wake Bob Gunnell, hali yake inaendelea vema.
Gunnell amesema kwamba familia ya bingwa huyo mwenye miaka 72 inahitaji faragha wakati akiendelea kupata matibabu dhidi ya maambukizi hayo ya mapafu.
Kwa muda mrefu bondia huyo wa zamani amekuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa 'Kutetemeka' (Parkinson) tangu alipostaafu ngumi mwaka 1984.

No comments:

Post a Comment