STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, January 2, 2015

Yanga waongoza Mapinduzi Cup, Simba kujiuliza kesho

Yanga X1HABARI kutoka Zanzibar kwa sasa kwenye mfululizo wa michuano ya Kombe la Mapinduzi,, Yanga wapo mbele kwa mabao 3-0 dhidi ya Jang'ombe.
Mabao yote yakiwekwa kimiani na Winga, Simon Msuva.
Mapema leo mchana KMKM na Mtende zilishindwa kutambiana kwa kutoka suluhu na Azam iliwabana mabingwa watetezi, KCCA ya Uganda na kufungana nao mabao 2-2.
Kesho kutakuwa na mechi mbili za kundi A, Simba ikitarajiwa kurudia tena dimbani baada ya jana kulala bao 1-0 kwa Mtibwa Sugar.
Simba itavaana na Mafunzo, wakati JKU yenyewe itavaana na Wakata Miwa wa Mtibwa Sugar.

No comments:

Post a Comment