STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, September 19, 2014

Jose Mourinho aanza mikwara yake England

http://cdn2.crhoy.com/wp-content/uploads/2014/06/Mou1.jpg 
SAA chache kabla ya kuvaana na mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya England, Jose Mourinho a.k.a Only Special' ameanza zake.
Meneja huyo wa Chelsea amedai hana tatizo katika kikosi chake na kwamba wapo kamili gado kuivaa  Manchester City Jumapili katika mchezo utakaochezwa katika Uwanja wa Etihad. 
Mourinho ameshuhudia kikosi chake kikishinda kila mchezo wa Ligi Kuu msimu huu lakini waligonga mwamba kwa Schalke Jumatano wakati walipolazimishwa sare. 
Hata hivyo, Mourinho anaamini Chelsea ina uwezo wa kuwafunga mahasimu wao hao katika mbio za ubingwa na kusisitiza wanajiamini kwa uwezo wao kuelekea katika mchezo huo. 
Kocha huyo kutoka Ureno, 51 amesema siku zote ni jambo zuri kucheza dhidi ya timu kubwa kwani inafanya kazi yake kuwa rahisi. 
Kocha huyo aliendelea kudai kuwa wanaiheshimu City kwasababu wanastahili lakini wao pia wanajiamini kufanya vyema katika mchezo huo.

No comments:

Post a Comment