STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, September 19, 2014

Wembley kutumika Nusu Fainali Ulaya 2020

https://www.daytona.co.uk/news_images/WEM_007936.jpgSHIRIKISHO la Soka Ulaya, UEFA limethibitisha kuwa Uwanja wa Wembley uliopo jijini London Uingereza ndiyo utakaotumika kwa mchezo wa nusu fainali na fainali ya michuano ya Ulaya 2020. 
Viwanja vya Hampden Park na Dublin Aviva vilivyopo jijini Glasgow, Scotland vinatarajiwa kutumika kwa ajili ya mechi za hatua ya 16 bora na mechi tatu za hatua ya makundi. 
Chama cha Soka nchini Uingereza,FA kilishinda nafasi hiyo baada ya Shirikisho la Soka la Ujerumani-DFB kujitoa muda mchache kabla ya kura za UEFA na kuamua kuhamishia nguvu zao katika kutafuta nafasi ya kuandaa michuano hiyo mwaka 2024. 
Michuano ya mwaka 2020 UEFA imefanya kuwa maalamu hivyo itaandaliwa katika viwanja 13 kutoka miji tofauti barani Ulaya. 
Mechi za robo fainali na tatu za hatua ya makundi zitaandaliwa jijini Munich, (Ujerumani), Baku (Azerbaijan), Roma (Italia) na St Petersburg (Urusi). 
Miji mingine itakayoandaa mechi 3 za makundi na moja ya mkondo wa pili ni Copenhagen (Denmark), Bucharest (Romania), Amsterdam (Uholanzi), Bilbao (Uhispania), Budapest (Hungary) na Brussels (Ubeljiji).

No comments:

Post a Comment