STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, September 20, 2014

Spurs walalamikia ubaguzi, wenyeji wao waomba radhi

Roberto Soldado
Patashika baina ya Spurs na Partizan

partizan banner
Bango lililoibua hisia za kibaguzi ambalo Spurs wamelalamikia UEFA
Jan Verthongen (R) challenges Partizan Belgrade"s Danko Lazovic UONGOZI wa klabu ya Tottenham Hotspurs limepeleka malalamiko yao Shirikisho la Soka la Ulaya, UEFA kufuatia kuonyeshwa kwa mabango yenye kulenga ubaguzi na mashabiki wa Partizan Belgrade. 
Meneja wa Spurs Mauricio Pochettino ameelezea bango hilo kama jambo lisilokuwa na heshima na lisilokubalika. 
Spurs walishindwa kutamba ugenini baada ya kulazimishwa suluhu na wenyeji wao katika Uwanja wa Partizani, nchini Serbia.
Maofisa wa Spurs waliwataarifu UEFA juu ya uwepo wa bango hilo kabla ya mapumziko na wajumbe wake walilipiga picha kama ushahidi baada ya mchezo huo. 
Mwaka 2007, Partizan walitolewa katika michuano ya Kombe la UEFA na kutozwa faini kwa vurugu wakati wa mchezo wa mkondo wa kwanza wa michuano hiyo dhidi ya Zrinjski Mostar.
Tayari uongozi wa klabu ya Partizan imeomba radhi kwa kitendo hicho kilichofanywa na mashabiki wao kupitia mabango hayo.

No comments:

Post a Comment