STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, September 20, 2014

Arsenal yaua ugenini, Welbeck atisha, Cisse aikoa Newcastle, Wanyama aizamisha Swansea akiangusha chozi uwanjani

Arsenal striker Danny Welbeck scores his first goal for the club
Alan Pardew
Kocha Allan Pardew akionyeshwa vipeperushi vya kutaka atimuliwe Newcastle kanbla ya Cisse kumuokoa kwa kufunga mabao mawili na kuambulia sare nyumbani
Papiss Cisse celebrates his second goal
Cisse akishangilia mabao yake jioni ya leo
Victor Wanyama (centre) celebrates his goal at the Liberty Stadium
Victor Wanyama akipongezqwa na wenzaake baada ya kuifungia Southampton bao pekee lililowapa ushindi ugenini dhidi ya Swansea City
ARSENAL wakiwa katika kiwango kizuri kabisa na kusahau kichapo chao cha Ligi ya Mabingwa Ulaya wameisambaratisha Aston Villa nyumbani kwao kwa kuwalaza mabao 3-0, huku Danny Welbeck akifunga moja ya mabao hayo.
Welbeck ambaye alikosa nafasi nyingi za kufungwa wakati Ze Gunners wakifa 2-0 nchini Ujerumani mbele ya Borussia Dortmund, alifunga bao la pili akimalizia pasi ya Mesut Ozil ambaye alitangulia kufunga bao la kwanza katika dakika ya 32.
Mshambuliaji huyo aliyesajiliwa toka Manchester United ndiye aliyemtengenezea bao hilo Ozil kabla na yeye kumtengenezea dakika mbili baadaye na kuifanya Arsenal kuwa mbele kwa mabao mawili.
Bao la tatu na la ushindi la vijana wa Arsene Wenger lilitokana na kijifunga kwa mchezaji wa Aston Villa, Ali Cissokho dakika ya 36.
Katika mechi nyingine za Ligi ya Engalnd, QPR ikiwa nyumbani ililazimisha sare ya mabao 2-2 na  Stoke City, sawa  na ilivyokuwa kwa Newcastle United iliyosubiri mtokea benchi Pappis Demba Cisse kufunga mabao mawili na kuepuka kipigi cha nyumbani dhidi ya Hull City, huku mashabiki wa Newcastle wakibeba vipeperushi vikitaka kocha Allan Pardew atimuliwe
Burnley ikiwa nyumbani ililazimishwa suluhu na Sunderland na Swansea ikijikuta ikipokea kipigo cha pili mfululizo baada ya kufungwa na Southampton ikiwa ni wiki moja tangu Chelsea walipowatoa nishai.
Bao pekee lililoizamisha Swansea iliyotoka kunyukwa mabao 4-2 liliwekwa kimiani na Mkenya Victor Wanyama dakia ya 80 huku nyota wa Swanseas Winfried Bony akilimwa kadi nyekundu baada ya kupata kadi za njano mbili katika pambano hilo.
Ushindi huo umeipaleka Southampton hadi kwenye nafasi ya pili nyuma ya Chelsea itakayoshuka dimbani kesho kuwakabili Manchester City uwanja wa ugenini.

No comments:

Post a Comment