STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, April 13, 2013

Prisons yazidi kukimbia janga la kushuka daraja


MAAFANDE wa Prisons Mbeya wamezidi kupigana kuepa janga la kushuka daraja baada ya kuinyoa Ruvu Shooting kwa mabao 2-0 katika pambano lililochezwa jioni ya leo mjini Mbeya.

Ushindi huo ni wa pili mfululizo baada ya Jumatano iliyopita kuicharaza Mgambo JKT, ulipatikana kwenye uwanja wa Sokoine na kuifanya Prisons kuchupa kwa nafasi moja toka nafasi ya 10 haid ya 9.
Hata hivyo bado Prisons ina kibarua cha kuhakikisha wanashinda mechi zao mbili zilizosalia dhidi ya JKT Ruvu na Kagera Sugar kujihakikishia kusalia Ligi Kuu msimu ujao.
Habari kutoka Mbeya zinasema kuwa Mabingwa hao wa zamani wa Tanzania walipata ushindi huo kwa magoli ya kipindi cha pili yaliyowekwa yote kimiani na mchezaji wake aliyekuw shujaa leo, Elias Maguli.Maguli alifunga bao la kwanza kwa shuti akiunganisha pasi murua ya mchezaji mwenzake katika dakika ya 53 kabla ya kuongeza jingine dakika tano baadaye kwa mkwaju wa penati baada ya beki mmoja wa Ruvu kuunawa mpira langoni mwake.
Kwa matokleo hayop Prisons imefikisha pointi 26 na kuishuka Mgambo katika nafasi ya tisa na kukalia wao nafasi hiyo.

Ligi hiyo inatarajiwa kuendelea tena kesho kwa pambano kati ya Azam na Simba litakalochezwa kwenye uwanja wa Taifa.

 Msimamo wa Ligi hiyo baada ya mechi za leo jioni;

                                        P     W     D    L     F     A     D     PTS
    1.  Young Africans     22     16    4     2    40   12    +28     52
    2.  Azam                     22     14    4     4    39   17    +22     46    
    3.  Kagera Sugar         22     10    7     5    25   18    +7       37     
    4.  Simba                     21     9     8     4     30   19   +11      35
    5.  Mtibwa Sugar        23      8     9     6     26   24    +2      33   
    6. Coastal Union         22     8     8     6     23    20    +3      32    
    7.  Ruvu Shooting       23     8     6     9     21     22     -1     30     
    8.  JKT Oljoro FC       23     7     7     9     22     27     -5     28     
    9. Tanzania Prisons     24     6     8    10    14     21     -7     26    
   10.JKT Mgambo          22     7     3    12    14     22     -8     24
   11.Ruvu Stars              21     6     4     11    19     34     -15   22
   12. Toto Africans        24     4     10    10    22    32     -10    22
   13.  African Lyon       23     5      4     14    16     35     -19   19
   14. Polisi Morogoro    23     3     10    10    11     21     -10   19    
             

No comments:

Post a Comment