STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, September 29, 2014

TID 'Mnyama' kufyatua na Tumi Molakane

MNYAMA TID, yupo hatua ya mwisho kukamilisha 'ngoma' yake mpya inayoenda kwa jina la 'Bongo' aliyomshrikisha rapa kutoka Afrika Kusini aiywao Tumi Molakane.
Kazi hiyo ya kwanza kwa TID kufanya na msanii huyo maarufu nchini mwake, imerekodiwa katika studio za B Records.
TID alidokeza kuwa kwa kitambo kirefu alikuwa akimwinda rapa huyo na kufanya naye mawasiliano kupitia mitandao ya kompyuta kabla ya kumzukia Dar na kuingia naye studio kufanya wimbo huo.
Staa huyo wa 'Zeze', 'Girlfriend', 'Nyota' na 'Voice of Prison' aliwataka mashabiki wake wajiandae kusikia 'kolabo' hiyo wakati akifanya mchakato wa kwenda Afrika Kusini baadaye ili kutengeneza video yake.
"ViDeo ifanywa Afrika Kusini ili kuleta ladha kulingana na ushiriki wa Tumi," alisema TID..

No comments:

Post a Comment