STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, September 29, 2014

Vumbi Ligi Mabingwa Ulaya kutimka kesho

http://content.mcfc.co.uk/~/media/Images/Home/News/Team%20News/2014%2015%20season/Home%20Games/Chelsea%2021%20September/Group%20celebration%20close%20up.ashx?h=451&w=800
Manchester City watakuwa kubaruani kesho
https://pbs.twimg.com/media/Byc8SnZIcAAUeg-.jpg:large
http://e0.365dm.com/14/03/768x432/Bayern-Munich-celebrate_3101995.jpg?20140315195810
Bayern Munich kuendeleza ubabe wake Ulaya kesho?

MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu ya England, Manchester City kesho inatarajiwa kutypa karata yake nyingine katika Ligi ya Mabingwa Ulaya wakati itakapowakaribisha As Roma ya Italia kwenye uwanja wa Etihad.
City itashuka nyumbani ikiwa na kumbukumbu ya kichapo cha bao 1-0 toka kwa Bayern Munich katika mechi yao ya raundi ya kwanza ya michuano hiyo.
Ikihanikizwa na ushindi wa ligi ya nyumbani City itahitaji ushinfi katika mechi ya kesho ya Kundi E ili kujiweka katika nafasi nzuri ya kuwa miongoni mwa timu zitakazosonga mbele katika makundi.
Mbali na mechi hiyo inayotarajiwa kuwa na upinzani mkali kesho pia kutakuwa na michezo mingine kadhaa likiwamo pambano la CSKA Moscow ya Urusi itakayokuwa nyumbani kuvaana na Bayern Munich.
Katika mchezo wa kwanza CSKA ilichabangwa mabao 5-1 na Roma, hali inayofanya iwe na kazi ya ziada kama iliyonayo City katika kundi hilo.
Makundi mengine yatashuhudia timu za PSG watakuwa nyumbani kuikaribisha Barcelona katika mechi ya Kundi F, huku APOEL Nicosia ya Cyprus itawakaribisha Ajax ya Uholanzi.
Vinara wa EPL, Chelsea watakuwa ugenini mjini Lisbon kucheza na wenyeji wao Sporting Lisbon, katika mechi ya Kundi G ambalo pia litakuwa na pambano jingine kati ya NK Maribor ya Slovania itakayocheza na Schalke 04 ya Ujerumani.
BATE Borislov ya Belarus watawaialika Athletic Bilbao ya Hispania na Shakhtar Donetsk ya Ukraine wakiwa wenyeji wa FC Porto ya Ureno, hizo zikiwa mechi za kundi H.
Kipute kingine cha michuano hiyo kwa makundi yaliyobakia kitaendelea siku ya Jumatano.

No comments:

Post a Comment