STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, February 12, 2015

Mama Muuza wa Shamsa bado kidogo tu

SHAMSA Ford, mmoja wa nyota wa filamu wa kike nchini, amewataka mashabiki wake wakae tayari kuipokea filamu yake mpya ya 'Mama Muuza' ambayo ipo hatua za mwisho ikirekebishwa kabla ya kuachiwa mtaani.
Akizungumza na MICHARAZO, Shamsa alisema filamu hiyo iliyotungwa na kutayarishwa na yeye mwenyewe ikiwa imewashirikisha wasanii kadhaa nyota akiwamo Haji Adam 'Baba Haji', itatoka Aprili.
"Nipo katika marekebisho ya mwishomwisho na nitaiachia 'Mama Muuza' miezi miwili ijayo kulingana na foleni iliyopo kwa wasambazaji," alisema.
Shamsa alisema kama ilivyokuwa kwa 'Chausiku' moja ya filamu iliyofanya vema kwa mwaka 2014, ndivyo 'Mama Muuza' itakavyokuwa kutokana na simulizi lake kubeba uhalisia wa maisha ya uswahili.
"Kama ilivyokuwa 2014 napenda mwaka 2015 uwe wenye raha na burudani kwa mashabiki wangu kupitia 'Mama Muuza'," alisema Shamsa.

No comments:

Post a Comment