STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, June 22, 2014

TFF yaridhia uchaguzi wa Simba kuendelea

malinzi
Rais wa TFF, Jamal Malinzi

SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limeridhia Uchaguzi Mkuu wa Simba uendelee kufanyika Juni 29 baada ya awali Rais wa shirikishiko hilo, Jamal Malinzi kunukuliwa akiupiga 'stop'.
Katika taarifa yake kwa wanahabari, TFF imesema baada ya kupokea na kuzingatia maombi ya Simba na kwa kuzingatia Ibara ya 26 ya Kanuni za Uchaguzi za TFF toleo la 2013 limeiruhusu klabu hiyo kuendelea na mchakato wa uchaguzi wao uliopangwa kufanyika Juni 29 mwaka huu.
 TFF inawahimiza wanachama wa klabu ya Simba kuwa watulivu na wafanye uchaguzi wao kwa amani.

No comments:

Post a Comment