STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, June 22, 2014

Nigeria yaua, Ghana yaibana Ujerumani, Klose akiweka rekodi



GERMANY: Neuer 6;  Boateng 6 (Mustafi 45mins 5.4), Mertesacker 6, Hummels  6, Howedes 6;  Lahm 7; Khedira 6.5 (Schweinsteiger 69mins 7),  Kroos 7; Mueller 6), Ozil 7, Goetze 7 (Klose 69mins 7.5).
GOALS: Gotze 51, Klose 71

GHANA: Dauda 7; Afful 6.5, Mensah 6.5, Asamoah 6, Boye 6; Boateng (J Ayew 51mins 6.5 ), Muntari 6, A Ayew 7.5, Atsu 7 (Wakaso 71mins 6); Rabiu 6 (Badu 77mins 6); Gyan 8 
GOALS: Ayew 54, Gyan 63
REFEREE: Sandro Ricci.













WAAFRIKA wameendelea kupumua katika Fainali za Kombe la Dunia timu za Nigeria na Ghana kufufua matumaini yao ya kucheza hatua ya 16 Bora kwa kupata matokeo ya kuridhisha mbele ya timu za Bosnia % Hezergonina na Ujerumani katika mechi zao zilizochezwa jana usiku.
Ghana ikiwa katika kiwango bora kabisa ilikaribia kuiadhiri Ujerumani baada ya kuongoza mabao 2-1 kabla ya mabingwa hao wa zamani wa Dunia kuchomoa bao 'jioni' kupitia mkongwe Miroslav Klose aliyeweka rekodi katika michuano hiyo kwa kufikisha bao 15 akilingana na Ronaldo de Lima.
Klose, 36 alifunga bao la kuisawazisha na kufanya matokeo kuwa 2-2 katika dakika ya 71 na kuiepushia Ujerumani kipigo chake cha kwanza baada ya muda mrefu kutokana na kufunikwa vilivyo na Black Stars.
Mechi hiyo ya kundi G ilichezwa mjini Fortaleza, Brazil ilishuhudia Waghana wakitanguliwa kufungwa bao dakika chache baada ya kutoka mapumziko kupitia kwa Mario Gotze aliyefunga dakika ya 51 kabla ya Ghana kuchomoa dakika tatu badaye kupitia kwa Andre Ayew 'Dede' .
Nyota wa Black Stars, Asamoah Gyan kuifungia timu yake bao la pili dakika ya 63 na kuonekana wazi Ujerumani walioifumua Ureno mabao 4-0 'itakufa' kwa Waafrika ikiwa ni mara ya kwanza tangu ilipofungwa mara ya kwanza na mwisho na timu za Afrika baada ya Algeria kuwatoa nishai 1982.
Hata hivyo Klose akaisawazishia Ujerumani bao hilo dakika ya 71 na kumfanya kumfikia Ronaldo wa Brazil ambaye ameshaachana na soka muda mrefu, huku pambano hilo likishuhudia pia beki wa Arsenal, Per Mertesacker ametimzia mechi 100 za kuichezea Ujerumani.
Katika mechi nyingine ya kusisimua Nigeria iliondoa 'gundu' la kutowahi kushinda katika fainali hizo tangu mwaka 1998 nchini Ufaransa baada ya kuilaza Bosnia kwa bao 1-0 na kufufua matumaini ya kuingia 16 Bora ikifikisha pointi 4 katika kundi lake.
Bao pekee la Peter Odemwingie la dakika ya 29 ya pambano hilo liliifanya waafrika kupumua kutokana na matokeo mabaya iliyopata timu zao Cameroon ikiondoshwa na Ivory Coast na Ghana zikipumulia mashine katika makundi yao katika kuwania kutinga raundi ya pili ya fainali hizo za Brazil.
Katika mechi ya mapema jana usiku, Argentina ikiwa na 'mchawi' wake, Lionel Messi ilijihakikishia kucheza 16 Bora baada ya kuilaza Iran bao 1-0 katika pambano la kundi F.
Argentina imefuzu kutokana na kupata ushindi wa pili mfululizo katika mechi ambayo ilioneikana kama ingeisha kwa suluhu kabla ya Messi kufunga bao la 'miujiza' dakika ya 90 na kuibeba Argentina ambayo sasa itamalizana na Nigeria wiki inayoanza kesho.

No comments:

Post a Comment