STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, February 22, 2014

Mtibwa Sugar yaona mwezi yainyuka Ashanti, Mgambo haikamatiki

Ashanti United waliyolazwa na Mtibwa Sugar
Mtibwa Sugar iliyoona mwezi
Oljoro JKT waliogeuzwa asusa na Mgambo mjini Arusha
Mgambo inayoendelea kugawa dozi kwa wapinzani wao katika Ligi Kuu
MABINGWA wa zamani wa kandanda nchini, Mtibwa Sugar leo imeona mwezi baada ya kupata ushindi wake wa kwanza katika mechi za duru la pili kwa kuinyoa Ashanti Utd wa mabao 2-1.
Mabao ya Mohammed Mkopi na Abdallah Juma ya kila kipindi yalitosha kuipa Mtibwa iliyokuwa uwanja wa nyumbani wa Manungu Complex pointi tatu muhimu vijana hao wa Mecky Mexime katika ligi hiyo inayozidi kuchanja mbuga.
Mshambuliaji wa zamani wa Simba, Mussa hassan Mgosi, alilimwa kadi nyekundu katika mchezo huo kabla ya timu yake kupata bao la ushindi lililofungwa na Abdallah Juma.
Katika mechi nyingine ya ligi hiyo, Rhino Rangers ikisafiri ugenini kuumana na wenyeji wa Kagera Sugar walishindiliwa bao 1-0 lililoifungwa na Suleiman Kibuta katika dakika ya nne na kuzidi kujiweka pabaya kwenye janga la kushuka daraja.
Nao Mgambo JKT ambao kwenye duru la pili wameonekana kuamka waliendeleza ubabe wao kwa kuichapa Oljoro JKT nyumbani kwao kwa mabao 2-1, mechi iliyochezwa kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid, jijini Arusha.

No comments:

Post a Comment