STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, February 22, 2014

Real Madrid yapanda kileleni Hispania


Real Madrid's Gareth Bale
MABAO matatu yaliyofungwa na Illaramendi katika dakika ya 34, Gareth Bale la dakika ya 72 na lile la Isco la dakika ya 81 yalitosha kuipaisha Real Madrid hadi kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu ya Hispania (La Liga) walipoifumua Elche mabao 3-0.
Madrid wakiwa uwanja wa nyumbani wa Santiago Bernabeu ilionyesha dhamira ya kupata ushindi kwa Illarramendi kufunga bao kwa pasi ya Pepe, bao lililodumu hadi mapumziko.
Bale mchezaji ghali kuliko wote katika usajili, alitupia bao la pili akimalizia kasi ya Xabi Alonso kabla ya Karim Benzema kumtengea Isco kufunga bao la tatu.
Kwa ushindi huo, Madrid imefikisha pointi 63 na kuziengua kileleni Barcelona na Atletico Madrid zenye pointi 60 kila moja ambazo zina mchezo mmoja mkononi, Barca wakitarajia kushuka dimbani muda mchache baadae ugenini dhidi ya Real Sociedad, huku wenzao wakitarajiwa kucheza kesho.




No comments:

Post a Comment