STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, October 3, 2013

Athuman Machuppa ampongeza na kumuonya Amisi Tambwe

Athuman Idd Machuppa akishangilia moja yha mabao yake alipokuwa akiichezae Vasalund ya Sweden

MSHAMBULIAJI nyota wa zamani wa klabu ya Simba na timu ya taifa, Taifa Stars, Athuman Machuppa amempongeza mfungaji mpya wa klabu hiyo Amisi Tambwe huku akimuonya ajipange zaidi ili asiye 'akafulia'.
Machuppa aliliambia MICHARAZO akiwa nchini Sweden kwamba japo hajamuona Tambwe akiwajibika uwanjani, lakini kwa sifa anazozisikia kuhusu mshambuliaji huyo Mrundi bila ya shaka ni 'bonge la Strika'.
Alisema kuanza kufumania nyavu mfululizo ni mwanzo mzuri kwa nyota huyo na kudai huenda anaisaidia Simba kurejesha heshima yake iwapo kama ataendelea kufunga.
Hata hivyo alisema kwa anavyoitambua Ligi ya Tanzania ni vyema mkali huyo akajipanga ili asije akaishia njiani kakma ilivyomtokea Mrundi mwenzake anayeichezea Yanga, Didier Kavumbagu.
"Kwa jinsi ninavyosikia simulizi zake ni wazi ni mmaliziaji mzuri na ataisaidia sana Simba na kwa kuanza kwake vyema na kuizoea mapema ligi ya Tanzania nampongeza na kumtaka aendeleze moto huo huo," alisema.
Machuppa aliongeza hata hivyo Tambwe hapaswi kulewa sifa  anazopewa na badala yake aongeze kasi ili aendelea kutamba na kuwapa raha wana Msimbazi sambamba na kutimiza ndoto zake za kuwa Mfungaji Bora.
"Unajua soka la Bongo halitabiriki, hata Kavumbagu alianza kwa kasi hiyo hiyo lakini mwisho wake umekuwaje, hivyo namsihi Tambwe asilewe sifa badala yake alinde kiwango chake kwa vile ligi ni ngumu," alisema.
Machuppa aliyemaliza mkataba wake wa kuichezea Vasby Utd inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza ya Sweden akitokea Vasalund pia ya nchini humo, alisema hata mashabiki wa Simba wanapaswa kumsaidia Tambwe.
Juu ya kitendo cha Tambwe kufunga mabao manne katika mechi moja, Machuppa alisifu ni jambo zuri linalovutia, ila hapaswi kupambwa kama ni kitu cha ajabu sana, wakati wapo wabongo waliowahi kufanya hivyo na pia kuna vijana wenye makali zaidi yake ila hawaaminiwi na makocha wao.
Kadhalika Machuppa alidokeza kusudio lake la kutaka kubadilisha uraia ili awe raia wa Sweden, akidai kwa sasa anasikilizia maombi yake aliyoomba Idara ya Uhamiaji wa nchi hiyo akitaka kufuata nyayo za Shekhan Rashid nyota mwingine wa Tanzania aliyewahi kutamba Simba na Taifa Stars.

No comments:

Post a Comment