STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, October 3, 2013

Mamlaka ya viwanja vya ndege (TAA) yajitosa bonanza la nyota wa Simba na Yanga Kisarawe


MAMLAKA ya viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) imejitosa kudhamini Bonanza la Soka litakalowahusisha nyota wa zamani wa klabu za Simba na Yanga litakalofanyika kesho (jumamosi) wilayani Kisarawe Pwani.
Bonanza hilo lililoandaliwa na klabu ya Kisarawe Veterani, linatarajiwa kufanyika Oktoba 5 kwenbye uwanja wa Bomani likishirikisha klabu 10 toka mkoa wa Dar na Pwani.
Mratibu wa bonanza hilo kutoka kampuni ya Mdau Entertainment, Mohammed Masenga alisema mamlaka hiyo imekubali kuwadhamini ili kufanikisha michezo hiyo ambayo itawakutanisha wachezaji waliowahi kutamba katika soka nchini.
Masenga, alisema kujitokeza kwa mamlaka hiyo ni faraja kwao kwa vile ni nadra kuziona taasisi za serikali zikijitokeza kusaidia michezo kama hiyo ya maveterani.
Aliongeza kuwa wanaishukuru mamlaka hiyo na kutaka taasisi nyingine za kiserikali kuiga mfano huo.
Kuhusu bonanza hilo, Masenga alisema maandaliai yake yanaendelea vyema na kwamba kivumbi kitatimka jumamosi kwa kuwashuhudia nyota hao wa zamani wa Simba na Yanga wanazozichezea timu shiriki za veterani.
Masenga alisema timu shiriki zitakazochuana katika bonanza hilo ni pamoja na Majohe Veterani, Pugu Veterani, Kigogo Veterani, Ukonga, Segerea ya akina Spear Mbwebwe na Willy Martin 'Gari Kubwa', Mbagala ya akina Yusuph Macho 'Musso', Kinyerezi Veterani, Bandari ya akina Kennedy Mwaisabula na Yobo.
Nyingine ni Vituka, New Ukonga na wenyeji Kisarawe Veterani na mshindi wa kwanza atanyakua seti nzima ya jezi, huku wa pili ataambulia 'bips' na wa tatu kubeba mpira mmoja.

No comments:

Post a Comment