STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, October 3, 2013

Liunda, Nkongo kushiriki kozi ya Futuro Addis Ababa

Liunda
Nkongo anayekimbia mbele

Na Boniface Wambura
MWAMUZI wa kimataifa wa zamani wa FIFA, Leslie Liunda na waamuzi Abdi Spud na Israel Nkongo ni miongoni mwa washiriki 30 walioteuliwa kuhudhuria kozi ya wakufunzi ya waamuzi ya FUTURO III itakayofanyika Addis Ababa, Ethiopia kuanzia Oktoba 5-10 mwaka huu.

Leslie Leonard Liunda, Abdi Soud Mohamed na Israel Nkongo Mujuni ndiyo watakaoshiriki katika kozi hiyo itakayoendeshwa na wakufunzi kutoka Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA).

Kozi hiyo pia itakuwa na washiriki kutoka nchi nyingine tisa za Afrika. Nchi hizo ni Gambia, Ghana, Kenya, Liberia, Nigeria, Seychelles, Sierra Leone, Somalia na Uganda.

No comments:

Post a Comment