STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, February 16, 2014

Messi aendelea kufanya maajabu Barcelona ikiua 6-0 nyumbani

Yebaaa! Watatukoma mwaka huu, Messi na Neymar wakipongezana jana
LIONEL Messi ameendelea kudhihirisha hana mpinzani katika medani ya ufumaniaji nyavu wakati usiku wa kuamkia leo alipotupia mabao mawili na kuisaidia Barcelona kuishindilia Rayo Vallecano kwa mabao mabao 6-0 katika mechi ya La Liga, Hispania.
Adriano Correia  alianza kuiandikia Barca bao dakika ya pili tu ya mchezo huo akimalizia kazi ya Pedro kabla ya Messi kuanza vitu vyake kwa kufunga bao la pili dakika ya 36  kwa pasi ya Fàbregas, mabao yalidumu hadi mapumziko.
Kipindi cha pili kilianza kwa kasi kwa wenyeji kuandika bao la tatu kupitia Alexis Sanchez aliyemalizia pasi ya Messi katika dakika ya 53.
Pedro aliiongezea Barca bao dakika tatu baadaye kwa kasi nzuri ya Fabregas ndipo Messi aliporejea tena kambani kwa kufunga bao lake la pili lililokuwa la tano kwa Barca akisaidiwa na Sánchez na msumari wa mwisho ukapigiliwa na Neymar dakika moja kabla ya kumalizika kwa mchezo huo na kuirejesha Barcelona kileleni ikiitoa Atletico Madrid waliokuwa wamekaa baada ya jana kushinda mabao 3-0 dhidi ya Real Valladorid.
Timu zote zimelingana pointi zikiwa na 60 kila mmoja ila zinatofautisha uwiano wa mabao ya kufunga na kufungwa, huku wakifutiwa kwa karibu na Real Madrid ambayo itashuka dimbani leo ugenini dhidi ya Getafe.
Katika mechi nyingine iliyochezwa jana Levante ilishinda nyumbani bao 1-0 dhidi ya Almeria na Celta Vigo imepata ushindi wa mabao 2-0 ugenini leo Jumapili dhidi ya wenyeji wao Villarreal.

No comments:

Post a Comment