STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, February 16, 2014

Inter Milan yaichabanga Fiorentina kwao

Kitu! mpira ukielekea wavuni mkwa wenyeji Fiorentina
Palacio akishangilia bao lake

MABINGWA wa zamani wa Ulaya, International Milan usiku wa kuamkia leo wameikwanyua Fiorentina ikiwa nyumbani kwao kwa kuilaza mabao 2-1 na kuzidi kuipumulia nyuma yake katika msimamo wa Ligi Kuu ya Italia (Seria A).
Inter walianza kuwashtukiza wenyeji wao kwa kufunga bao la kuongoza dakika ya 34 kupitia Palacio na kudumu hadi mapumziko.
Kipindi cha pili iliwachukua dakika mbili tu kwa Fiorentina kurejesha bao hilo kupitia kwa Cuadrado aliyemalizia kazi nzuri ya Fernandez.
Hata hivyo walikuwa ni wageni waliojihakikishia ushindi baada ya Icardi kuifungia Inter bao la pili na la ushindi dakika ya 65 kwa kumalizia kazi nzuri iliyofanywa na Nagatomo.
Kwa ushindi huo, Inter imefikisha pointi39 tano nyuma ya wapinzani wao hao waliopo nafasi ya nne wakiwa na pointi 44.
Kivumbi cha ligi hiyo kinatarajiwa kuendelea tena leo kwa michezo kadhaa likiwamo lile la vinara wa ligi hiyo Juventus itakayoumana na Chievo mjini Turin.

No comments:

Post a Comment