STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, January 18, 2012

Coastal Union yakuna kichwa kwa Simba

UONGOZI wa klabu ya soka ya Coastal Union ya Tanga, umedai pambano lao la awali la duru la pili la Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Simba litakalofanyika wiki ijayo linawapasua vichwa wakitafakari mbinu za kuweza kuwapa ushindi wa mchezo huo.
Coastal iliyorejea Ligi Kuu msimu huu, itakwaruzana na Simba katika pambano la marudiano litakalofanyika Jumatano ijayo kwenye uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Afisa Habari wa timu hiyo, Eddo Kumwembe, alisema kuwa kuanza duru la pili kwa kuumana na Simba ni mtihani mgumu ambao unawafanya wajipange vema ili kufanya vema kabla ya kufunga safari kuwafuata Mtibwa Sugar kwenye dimba lao la nyumbani.
Kumwembe, alisema uongozi wao upo makini na pambano hilo kwa vile wanataka washinde ili kujiweka katika mazingira mazuri ya kuondoka nafasi za mkiani mwa msimamo wa ligi hiyo.
"Kuanza na timu kubwa kama Simba ni mtihani unaortuchanganya akili kwa sasa, tukijipanga kwa umakini mkubwa kuona tunaibuka na ushindi kabla ya kwenda kuvaana na Mtibwa huko Manungu," alisema Kumwembe.
Alisema lengo la uongozi wao ni kuona Coastal Union, inatoka maeneo ya mkiani na kuwa miongoni mwa timu za nafasi za juu, hasa baada ya kuongeza nyota kadhaa katika kikosi chao wakati wa usajili wa dirisha dogo.
"Tunataka Coastal ifanye vema kwenye duru hili, ndio maana hata kocha wetu aliamua kufuta mechi yetu dhidi ya Gor Mahia ya Kenya kusudi arekebishe mambo kutokana na kuwa nyuma ya mipango yake," alisema Kumwembe.
Kumwembe aliongeza, kwa kikosi walichonacho sasa ni wazi timu yao itarejesha makali yake ya zamani yaliyoipa ubingwa wa nchi.
Nyota waliongezwa katika kikosi cha Coastal ni Mkenya Edwin Mukenya, Ally Shiboli, Wanigeria Felix Amechi na Samuel Temi na wakali wengine waliokuwa katika usajili w awali wakiwemo washambuliaji Ben Mwalala na Aziz Gilla.

Mwisho

No comments:

Post a Comment