STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, January 18, 2012

Banana, JB, Riyama waja na DNA




MWANAMUZIKI nyota nchini, Banana Zorro anatarajia kuibukia kwenye filamu kupitia kazi mpya iitwayo DNA aliyoigiza na nyota wa fani hiyo kama Riyama Ally, Jacob Stephen 'JB' na Sabrina Rupia maarufu kwa jina la 'Cathy'.
Kazi hiyo mpya inayohusiana na masuala ya kijamii na namna hila zinavyoweza kufanywa katika upimaji wa vinasaba na kuleta mtafaruku, inatarajiwa kuingia sokoni wakati wowote kuanzia sasa.
Kwa mujibu wa taarifa za wasambazaji, ni kwamba kama anavyotamba katika muziki, Banana ambaye ni mtoto wa gwiji wa muziki wa dansi nchini, Zahir Ally Zorro ameonyesha umahiri mkubwa pia katika filamu.
"Ndani ya DNA, Banana Zorro kathibitisha kuwa habahatishi. Ameshawahi kucheza filamu kadhaa nyuma ikiwemo ya 'Handsome', na humu pia amefanya vizuri sana," imeelezwa katika taarifa hiyo.
Katika hatua nyingine, filamu mpya ya 'I Hate My Birthday' ya Vincent Kigosi 'Ray' inatarajiwa kuanza kusambazwa keshokutwa ambapo ndani yake wameshiriki nyota kadhaa kama Irene Paul na Aunty Ezekiel.

No comments:

Post a Comment